0% found this document useful (0 votes)
586 views32 pages

S4 Kiswahili

Uploaded by

ivanoyel003
Copyright
© © All Rights Reserved
We take content rights seriously. If you suspect this is your content, claim it here.
Available Formats
Download as PDF, TXT or read online on Scribd
0% found this document useful (0 votes)
586 views32 pages

S4 Kiswahili

Uploaded by

ivanoyel003
Copyright
© © All Rights Reserved
We take content rights seriously. If you suspect this is your content, claim it here.
Available Formats
Download as PDF, TXT or read online on Scribd
You are on page 1/ 32

Ministry of Education

and Sports

HOME-STUDY

I O
N

4
R
S E
Published 2020

This material has been developed as a home-study intervention for schools during the
lockdown caused by the COVID-19 pandemic to support continuity of learning.

Therefore, this material is restricted from being reproduced for any commercial gains.

National Curriculum Development Centre


P.O. Box 7002,
Kampala- Uganda
www.ncdc.go.ug
SELF-STUDY LEARNING

FOREWORD

Following the outbreak of the COVID-19 pandemic, government of Uganda


closed all schools and other educational institutions to minimize the
spread of the coronavirus. This has affected more than 36,314 primary
schools, 3129 secondary schools, 430,778 teachers and 12,777,390
learners.

The COVID-19 outbreak and subsequent closure of all has had drastically
impacted on learning especially curriculum coverage, loss of interest in
education and learner readiness in case schools open. This could result in
massive rates of learner dropouts due to unwanted pregnancies and lack
of school fees among others.

To mitigate the impact of the pandemic on the education system in


Uganda, the Ministry of Education and Sports (MoES) constituted a
Sector Response Taskforce (SRT) to strengthen the sector’s preparedness
and response measures. The SRT and National Curriculum Development
Centre developed print home-study materials, radio and television scripts
for some selected subjects for all learners from Pre-Primary to Advanced
Level. The materials will enhance continued learning and learning for
progression during this period of the lockdown, and will still be relevant
when schools resume.

The materials focused on critical competences in all subjects in the


curricula to enable the learners to achieve without the teachers’
guidance. Therefore effort should be made for all learners to access and
use these materials during the lockdown. Similarly, teachers are advised
to get these materials in order to plan appropriately for further learning
when schools resume, while parents/guardians need to ensure that their
children access copies of these materials and use them appropriately.
I recognise the effort of National Curriculum Development Centre in
responding to this emergency through appropriate guidance and the
timely development of these home study materials. I recommend them for
use by all learners during the lockdown.

Alex Kakooza
Permanent Secretary
Ministry of Education and Sports

iii
ACKNOWLEDGEMENTS

National Curriculum Development Centre (NCDC) would like to express its


appreciation to all those who worked tirelessly towards the production of
home–study materials for Pre-Primary, Primary and Secondary Levels of
Education during the COVID-19 lockdown in Uganda.

The Centre appreciates the contribution from all those who guided
the development of these materials to make sure they are of quality;
Development partners - SESIL, Save the Children and UNICEF; all the
Panel members of the various subjects; sister institutions - UNEB and DES
for their valuable contributions.

NCDC takes the responsibility for any shortcomings that might be


identified in this publication and welcomes suggestions for improvement.
The comments and suggestions may be communicated to NCDC through
P.O. Box 7002 Kampala or email [email protected] or by visiting our
website at http://ncdc.go.ug/node/13.

Grace K. Baguma
Director,
National Curriculum Development Centre

iv
SELF-STUDY LEARNING

ABOUT THIS BOOKLET

Dear learner, you are welcome to this home-study package. This content
focuses on critical competences in the syllabus.

The content is organised into lesson units. Each unit has lesson activities,
summary notes and assessment activities. Some lessons have projects
that you need to carry out at home during this period. You are free to use
other reference materials to get more information for specific topics.

Seek guidance from people at home who are knowledgeable to clarify in


case of a challenge. The knowledge you can acquire from this content can
be supplemented with other learning options that may be offered on radio,
television, newspaper learning programmes. More learning materials can
also be accessed by visiting our website at www.ncdc.go.ug or
ncdc-go-ug.digital/. You can access the website using an internet enabled
computer or mobile phone.

We encourage you to present your work to your class teacher when


schools resume so that your teacher is able to know what you learned
during the time you have been away from school. This will form part of
your assessment. Your teacher will also assess the assignments you will
have done and do corrections where you might not have done it right.

The content has been developed with full awareness of the home learning
environment without direct supervision of the teacher. The methods,
examples and activities used in the materials have been carefully selected
to facilitate continuity of learning.

You are therefore in charge of your own learning. You need to give
yourself favourable time for learning. This material can as well be used
beyond the home-study situation. Keep it for reference anytime.

Develop your learning timetable to ca ter for continuity of learning and


other responsibilities given to you at home.

Enjoy learning

v
SELF-STUDY LEARNING

Term 2&3
Kiswahili Self-study Material Kidato cha nne

MadaKuu 1: Mnyambuliko wa vitenzi

Funzo/somo: Hali ya kutenda, hali ya kutendwa, hali ya kufanyia/kutendea, kutendena,


kutendeana, kutendesha, kufanyafanya na Kutendeka.
Umilisi: Baada ya kujifunza funzo hili utaweza, kunyambua vitenzi katika hali ya kuten-
da, kutendea, kutendewa, kutendesha, kutendeana, kutendana, kutendatenda na ku-
tendeka.
Utahitaji vifaa kama; muda, daftari, kalamu, n.k

Utangulizi
Je, unajua kuwa kunyambua kitenzi ni kuzalisha neno au maneno mapya? Umeshawahi
kunyambua vitenzi vya Kiswahili na kuzalisha maneno mapya kutokana na vile vitenzi vya
awali? Katika somo hili utajifunza kuhusu hali mbalimbali za mnyambuliko wa vitenzi.
Maagizo: Tafuta pahali mwafaka kusoma makala haya. Utafanya mazoezi na shughuli zote
zilizomo. Kumbuka kuwa baadhi ya shughuli zinaweza kuchukua muda mrefu. Soma maagizo
kwa makini kabla ya kufanya zoezi/shughuli husika.

Mnyambuliko wa vitenzi
Vitenzi huwa katika hali/kauli mbalimbali kama zinavyooneshwa hapo chini:
Shughuli 1.1: Kutambua hali za mnyambuliko wa vitenzi
1. Soma kwa sauti na kisha utafakari juu ya hali/kauli zinazooneshwa hapo chini.
2. Taja vitenzi ambavyo vimenyambuliwa katika hali/kauli zifuatazo.

Hali ya kutenda
Inahusisha upande mmoja k.m;
Ninasoma kitabu.

Hali ya kutendea/kufanyia
Hii inahusisha pande mbili ambapo upande mmoja unafanya jambo kwa upande mwingine.
K.m; Mama anapigia baba simu.

Hali ya kutendewa
Katika kauli hii, upande mmoja unatenda jambo kwangu au kwa mtu mwingine. K.m;
Nimepigiwa simu au Baba atapigiwa simu.

1
KISWAHILI | SENIOR FOUR

Hali ya kutendesha
Hii ni hali ya kusababisha jambo litendeke. K.m Mama anamlisha mtoto. Hapa mama
anamfanya mtoto ale chakula.

Hali ya kutendana
Hapa upande mmoja unatenda na wa pili pia unatenda. Kwa hivyo wanatendana. Hali
ya kutendana ni pale ambapo mtu au mnyama humtendea mwingine kitendo kilekile ali-
chotendewa K.m; Ninampenda naye ananipenda –Tunapendana.

Hali ya kutendeana
Katika hali hii, watu wanafanyiziana vitendo. Kwa mfano, Akello akimpigia simu Chemu-
tai naye Chemutai akampigia simu Akello, watakuwa wanapigiana simu.

Hali ya kutendatenda
Hii ni hali ya kurudiarudia kitendo mara kwa mara. K.m; Tangu Virusi vya Korona viingie
nchini Uganda, watu wananawanawa mikono yao.

Hali ya kutendeka
Hapa jambo linatokea labda bila kuingiliwa na upande wowote.k.m; Kitabu kimeanguka.
Au Msichana huyu alirembeka.

Zoezi 1.1: Kujaza jedwali

1. Jaza jedwali lifuatalo kwa usahihi

K i t e n z i ( - kufanyia k u t e n d e - k u t e n d e - kutendana kutendeka


tenda) wa sha
Soma somea
Cheza
Jenga
Piga
Uma
Umba

2
SELF-STUDY LEARNING

2. Chagua jibu sahihi kutoka kwa mabano kukamilisha sentensi zifuatazo:


(bebwa, fundisha,kumbatiana)

Wasichana wame. . . . . . . Mtoto ame . . . . . na baba Mwalimu ana. . . . . . . . .

Muhtasari wa mada

Je, unakumbuka kuwa katika mada hii umejifunza kuhusu, kunyambua vitenzi katika hali
ya kutenda, kutendea, kutendewa, kutendesha, kutendeana na kutendana, kutendaten-
da na kutendeka? Ujuzi huu utakusaidia kuimarisha umilisi wako wa lugha ya Kiswahili.

Mada Kuu 2: Ufahamu

Funzo/somo: Kusoma makala na kujibu maswali


Umilisi: Baada ya kujifunza somo hili utaweza;
i. Kusoma makala mbalimbali na kujibu maswali husika.
ii. Kutambua msamiati mpya na kuutumia katika sentensi.
iii. Kutambua funzo au ujumbe katika makala ya ufahamu.
Utahitaji vifaa kama; muda, daftari, kalamu, n.k

Utangulizi

Unajua kuwa wanafunzi wengi hawafanyi vizuri sana katika kujibu maswali ya ufahamu?
Tatizo hili hutokana na ukosefu wa makini wakati wa kusoma ufahamu na hata wakati wa
kuyajibu maswali yenyewe. Je, wewe kama mtahiniwa unafaa kufanya yapi ili ufanye vizuri
katika sehemu ya ufahamu? Katika somo hili utajifunza kanuni mbalimbali unazostahili
kufuata ili ufue dafu katika ufahamu.
Maagizo: Tafuta pahali mwafaka kusoma makala haya. Utafanya mazoezi na shughuli zote
zilizomo. Kumbuka kuwa baadhi ya shughuli zinaweza kuchukua muda mrefu. Soma maagizo
kwa makini kabla ya kufanya zoezi/shughuli husika.

3
KISWAHILI | SENIOR FOUR

Ufahamu

Ufahamu ni uwezo wa kusoma na kuelewa maneno au habari ambayo imeandikwa. Ili


mwanafunzi kuelewa taarifa ya habari lazima aisome zaidi ya mara moja. Pia, anafaa
kusoma maswali zaidi ya mara moja. Maswali ya ufahamu huwa yanahitaji; majibu yan-
ayopatikana katika matini husika, kueleza maana ya msamiati, majibu ya kutoa maoni
yako au kupendekeza suluhisho fulani na kuelezamafunzo unayopata baada ya kusoma
matini fulani.
Shughuli 2.1: Kutambua utaratibu wa ufahamu

1. Soma kanuni au utaratibu ufuatao ili uweze kumakinika katika kujibu maswali ya
ufahamu.

Utaratibu wa ufahamu

a. Soma matini ya ufahamu mara ya kwanza. Kusoma huku kutakuwezesha kuelewa


maudhui ya ufahamu kwa kiasi fulani.
b. Yasome maswali yaliyoulizwa.
c. Soma matini tena na kwa makini.
d. Rudia kusoma maswali.
e. Lisome kila swali kwa makini.
f. Tafuta jibu la swali hilo katika ufahamu. Ni vizuri kupigia mstari au kuweka alama
katika sehemu ambayo umepata jibu la swali.
g. Unapoulizwa kupendekeza kichwa mwafaka cha ufahamu, sharti uweze kugundua
ni ujumbe upi uliopewa umuhimu zaidi katika makala/ufahamu.
h. Unapoulizwa swali linalohitaji maana ya neno au sentensi, unatakiwa usome neno
hilo au sentensi hiyo ukizingatia jinsi ambavyo imetumika.

Zoezi 2.1: Kusoma matini na kujibu maswali

1. Soma kifungu kifuatacho na kisha ujibu maswali yaliyo chini.


Wambuzi ni kijana ambaye anapenda kupanda miti kila siku na kurukia chini. Baba yake
alimkataza mchezo mbaya wa kupandapanda miti na kurukarukia chini. Alimwambia
kuwa anaweza akaruka na kuanguka chini vibaya. Mtu akianguka chini vibaya anaweza
akapoteza viungo vyake. Mojawapo ya viungo hivyo ni midomo, meno ulimi n.k. Alim-
wambia kuwa mtu akipoteza ulimi hataweza kutamka irabu zote. Akipoteza midomo ha-
taweza kutamka irabu /o/ na /u/ pamoja na konsonanti /b/, /p/, /m/, na /w/. Pia, alim-
wambia kuwa akipoteza meno ya mbele na mdomo wa chini atashindwa kutamka sauti,
/f/ na /v/. Akipoteza ncha ya ulimi na meno ya mbele atashindwa kutamka sauti, /th/
na /dh/. Aidha, alimweleza kuwa mtu akipoteza ulimi mbali na kushindwa kutamka irabu
pia atashindwa kutamka sauti za konsonanti kama /ch/, /l/, /n/, /s/, /t/, /sh/ na /z/.
Mbali na kumkataza kupanda miti, alimkataza kupigana kwa sababu anaweza akapig-
wa ngumi na kupoteza midomo, meno au hata ulimi. Pia, alimwambia kuwa asiposugua
meno kila anapoamka asubuhi na kabla ya kulala, meno yanaweza kuoza na kusababisha
kuong’olewa. Yaking’olewa atashindwa kutamka sauti za meno.

4
SELF-STUDY LEARNING

Jibu maswali haya kutokana na ufahamu.


1. Ni nani ambaye anapenda kupanda miti na kurukia chini?
2. Je, baba yake alimkataza nini?
3. Mtu akipoteza ulimi anashindwa kutamka sauti zipi?
4. Je, mtu akipoteza meno ya mbele na mdomo wa chini atashindwa kutamka sauti
zipi?
5. Kwa nini baba yake alimkataza kupigana?
6. Wambuzi aliambiwa asiposugua meno kila asubuhi na kabla ya kulala ni nini kin-
achoweza kutokea?
7. Eleza maana ya maneno yafuatayo kama yalivyotumiwa katika kifungu.
a. kuruka b. viungo c. poteza d. ncha e. sugua f. ng’olewa
Shughuli 2.2: Kutafuta makala ya ufahamu
1. Kwa kutumia mtandao/intaneti, kitabu cha kiada au gazeti, tafuta makala ya ufa-
hamu, uyasome na kisha ujibu maswali yake.
2. Sikiliza makala kwa redio au runinga na kisha ujibu maswali yanayoulizwa kuhusu
makala hayo.

Muhtasari wa mada

Je, unakumbuka kuwa katika mada hii umejifunza kuhusu, kusoma makala mbalimbali ya
ufahamu na kujibu maswali? Ujuzi huu utaimarisha uelewa wako wa lugha ya Kiswahili.

Mada ya tatu: Uandishi wa insha

Funzo/somo la kwanza: Mahitaji ya uandishi wa insha

Umilisi:

Baada ya kujifunza somo hili utaweza;


i) Kutambua mahitaji ya uandishi wa insha.
ii) Kutambua makosa wanayofanya wanafunzi wakati wa kuandika insha.
Utahitaji vifaa kama; muda, daftari, kalamu, n.k

Utangulizi
Unajua kuwa ili mwanafunzi aweze kuandika insha nzuri, sharti aelewe na kufuata sheria za
uandishi wa insha? Je, unajua kuwa wanafunzi wengi hufanya makosa katika uandishi wa
insha bila kujua? Katika somo hili utajifunza kanuni mbalimbali unazostahili kufuata katika
uandishi insha nzuri ili kuepuka kufanya makosa.
Maagizo: Tafuta pahali mwafaka kusoma makala haya. Utafanya mazoezi na shughuli zote
zilizomo. Kumbuka kuwa baadhi ya shughuli zinaweza kuchukua muda mrefu. Soma maagizo
kwa makini kabla ya kufanya zoezi/shughuli husika.

5
KISWAHILI | SENIOR FOUR

Uandishi wa Insha

Kuna aina nyingi za insha ambazo mwanafunzi wa kidato cha nne anatakiwa kuandika.
Ili uweze kuandika insha hizo vizuri, sharti uelewe na uzifuate sheria za utunzi wa insha.

Shughuli 3.1: Kukariri sheria za Uandishi wa insha

1. Kariri sheria zifuatazo zinazofaa kufuatwa katika utunzi wa insha;


• Hati/mwandiko mzuri unaosomeka kwa urahisi.
• Urefu wa kutosha wa insha.
• Lugha sanifu isiyo na makosa ya kisarufi.
• Matumizi mazuri ya msamiati au uteuzi mwafaka wa maneno. Lazima utumie ma-
neno au sentensi fupifupi zinazoeleweka.
• Upambaji wa lugha kwa kutumia tamathali mbalimbali za usemi kama vile; meth-
ali, tashbihi, istiara, n.k.
• Mtiririko mzuri wa mawazo- mwanzo hadi mwisho, n.k.

Ulikuwa unajua?
Wanafunzi wengi hufanya makosa katika uandishi wa insha. Yakariri mako-
sa yafuatayo na uyalinganishe na yale unayoyajua :

1. Kutosoma insha mara tu baada ya kuiandika. Ni vizuri kusoma insha ili kuyasahi-
hisha makosa uliyoyafanya wakati wa kuandika.
2. Kutumia maneno usiyokuwa na uhakika kuyahusu. Badala yake, unafaa kuuliza au
kufanya utafiti kuyahusu maneno yale.
3. Kukatakata maneno k.m angesoma, nilipo fika badala ya nilipofika, aliye kuita
badala ya aliyekuita.
4. Kuyashikanisha maneno k.m. Kwasababu badala ya kwa sababu Kwanini badala
ya kwa nini, n.k.
5. Maendelezo mabaya k. minchibadala ya nchi, kua badala ya kuwa, tama badala
ya tamaa, n.k.
6. Kutumia sentensi ndefu na za kuchosha. Mwanafunzi anashauriwa kutumia sen-
tensi fupi na sahihi.
7. Matumizi ya maneno yasiyo ya Kiswahili. Maneno yasiyo ya Kiswahili yatabeba
adhabu kali katika kutuza alama.
8. Matumizi ya maneno ya mkato kama dadangu, mamaye yaepukwe.

Funzo la pili: Kutambua aina za insha

Umilisi: Baada ya kujifunza somo hili, utaweza:


i. Kutambua aina mbalimbali za insha.
Utahitaji vifaa kama; muda, daftari, kalamu, n.k

Utangulizi
Kufikia kidato cha nne, mwanafunzi anatakiwa kutambua insha mbalimbali ambazo ana-
takiwa kuandika katika mtihani wa taifa. Insha hizo zimegawanywa katika aina mbalim-
bali. Katika somo hili, utajifunza namna ya kuainisha insha mbalimbali.

6
SELF-STUDY LEARNING

Shughuli 3.2: Kutambua aina za insha


1. Fanya utafiti kuhusu aina zifuatazo za insha na uandike maelezo machache kuhu-
su namna zinavyoandikwa.

Aina za insha

Kufikia kidato cha nne, mwanafunzi anastahili kuwa amejifunza namna ya kuandika in-
sha mbalimbali. Insha hizo ni kama zifuatazo:
a. Insha za mada teule
b. Insha za mwongozo
c. Insha za mjadala
d. Insha za methali mara nyingi hizi huwa chini ya insha za mada teule.
e. Insha za barua
f. Insha za mazungumzo
g. Insha za ratiba
h. Insha za hotuba
i. Insha za kumbukumbu
j. Insha za shajara
k. Insha za picha
l. Insha za ripoti
m. Insha za matangazo
n. Insha za maelekezo, n.k.

Insha ya mada teule

Insha hii huhitaji mwanafunzi kutoa hoja za jambo fulani. Katika insha hii, mwanafunzi
anatakiwa kuandika mambo ya ukweli wala si yale ya kubuni. Soma mfano ufuatao wa
insha ya mada teule.
1. Madhara ya ugonjwa wa COVID-19 nchini Uganda.

Kichwa: COVID-19 NI JANGA KWA TAIFA

Utangulizi: Eleza kwa ufupi jinsi ugonjwa wa COVID-19 umekuwa janga kwa taifa la
Uganda.
Mwili: Eleza madhara ya Ugonjwa wa COVID -19. K.m,
-Ugonjwa wa COVID-19 umesababisha watu kupoteza kazi zao
-Watu wameshindwa kukimu mahitaji yao na ya wale wanaowategemea.
-Gharama imeongezeka wa taifa na jamii, k.m, kununua, dawa, vitakasa mikono, bara-
koa, n.k.
-Umaskini kwa kuwa watu hulazimishwa kubaki nyumbani.
-Uchumi huzorota.
-Husababisha vifo, n.k.

7
KISWAHILI | SENIOR FOUR

Tamati/mwisho: Kutahadharisha watu wajiepushe na janga la COVID-19 kwa kuvaa


barakoa, kunawa mikono, kutakasa mikono, kujitenga, kutojishika katika macho, puani,
mdomoni, n.k.
Shughuli 3.3: Kuandika insha ya mada teule
Andika insha isiyopungua maneno 350 wala kuzidi 400 kuhusu mojawapo ya
vichwa vifuatavyo;
a. Siku ambayo sitaisahau daima.
b. Chanzo cha ajali za barabarani nchini Uganda.
c. Athari za janga la COVID-19 (Virusi vya Korona) nchini Uganda.
d. Haba na haba hujaza kibaba.
e. Elimu ya msichana ni bora kuliko ya mvulana. Jadili.
f. Mali ni bora kuliko elimu. Jadili.

Funzo la tatu: Kuandika insha barua


Umilisi: Baada ya kujifunza somo hili, utaweza:
i). Kuandika aina mbalimbali za barua
Utahitaji vifaa kama; muda, daftari, kalamu, n.k.

Utangulizi
Kuna aina mbalimbali za barua ambazo mwanafunzi wa kidato cha nne anatakiwa ku-
ziandika. Insha hizo za barua ni muhimu sana kwa sababu zinamsaidia mwanafunzi
katika maisha yake ya baadaye. Katika somo hili, utajifunza namna ya kuandika aina
mbalimbali za barua.

Mifano ya insha mbalimbali

Insha ya barua
Kuna aina mbili za barua, yaani; barua ya kirafiki na barua rasmi

Barua ya kirafiki
Hii huandikwa kwa rafiki au hata mtu wa familia. Unaweza kumwandika ndugu au rafiki
yako ili kumjulia hali, kumpongeza, kumpa pole, kumwalika katika sherehe, kumwomba
msaada, n.k.
Barua ya kirafiki huwa na sehemu hizi;
Anwani ya mwandishi, sehemu ya mwandikiwa, utangulizi/aya ya kwanza, mwili/kiwili-
wili, mwisho/tamati na jina la mwandishi.
Ebu soma mfano wa barua ya kirafiki hapo chini:

8
SELF-STUDY LEARNING

SHULE ZA UPILI BANDA,


S.L.P 271
KAMPALA-UGANDA
26. AGOSTI.2020

Mpendwa baba,
Shikamoo baba! Mimi ni mzima. Natumai pia nyinyi hamjambo huko nyumbani?

Safari yangu kutoka nyumbani hadi Kampala ilikuwa nzuri. Tulisafiri usiku kucha tukaf-
ika asubuhi na mapema.

Shughuli za muhula mpya zimeanza. Masomo ya kidato cha nne ni magumu kiasi lakini
tunajitahidi ipasavyo.

Nimekuandikia barua hii kukuomba pesa za matumizi kwa sababu pesa ambazo ulinipa
nilizitumia kununua vitabu na vifaa vingine vya kutumia hapa shuleni.

Natarajia kuwaona mwezi wa desemba tutakapokuwa likizoni. Msalimu mama, bibi,


babu na kaka.

Mwanao mpendwa,

Karangwa Zabuloni

Zoezi
Mwandikie rafiki yako barua umweleze jinsi ulivyotumia likizo ya COVID-19.

Barua rasmi
Hizi huandikwa kwa shughuli rasmi au za kiofisi kama vile; kuomba nafasi ya kazi, kuom-
ba nafasi ya masomo, kuomba msamaha, n.k. Barua rasmi ina sehemu zifuatazo; anwani
ya mwandishi-hii hujumuisha makao yake na sanduku la posta (S.L.P), anwani ya mwan-
dikiwa, nani anayeandikiwa kama Kwa Bibi/Bwana, lengo/kichwak.m, KUH: KUOMBA
NAFASI YA KAZI, utangulizi (aya hii huwa fupi), mwili wa barua, tamati (hii ni aya ya
mwisho), jina la mwandishi sanasana huwa hivi:
Wako mwaminifu,
(Sahihi/saini)
Jina
Angalia mfano wa barua rasmi.

9
KISWAHILI | SENIOR FOUR

SHULE ZA UPILI YA YAMOTO,


S.L.P 271

LUWERO-UGANDA
29. SEPTEMBA.2020

MWALIMU MKUU SHULE YA MSINGI WA ZINUNULA,


S.L.P 45,
WOBULENZI
Kwa Bwana/Bibi,
KUH/MINT/YAH: MAOMBI YA NAFASI YA KAZI YA UALIMU
Kwa heshima kubwa ninaomba nafasi ya kazi ya kufundisha somo la Kiswahili katika
shule yako.
Mimi ni mwanamume wa umri wa miaka ishirini. Nimehitimu elimu ya shule ya sekondari
katika Shule ya upili ya Yamoto wilayani Luwero. Katika shule hiyo, nilikuwa na bidii,
uajibikaji na nidhamu ya hali ya juu. Ninaweza kufundisha Kiswahili na Kiingereza vizuri
sana.
Ukinipa nafasi hii, nitafanya kazi kwa bidii na uajibikaji. Pamoja na barua hii, nimeam-
batanisha na vyeti vyangu.
Nitashukuru sana ombi langu likipokelewa vizuri.
Wako mwaminifu,
................
Bahati Musa

Zoezi
1. Andika barua kwa Mwalimu mkuu ukimwomba nafasi ya kujiunga na kidato cha
tano katika shule yake.
2. Andika barua kwa mwalimu ukimwomba msamaha kwa kutohudhuria masomo bila
kumjulisha mapema.

Funzo la nne: Kuandika insha ripoti


Umilisi: Baada ya kujifunza somo hili, utaweza:
i). Kuandika aina mbalimbali za ripoti

10
SELF-STUDY LEARNING

Utahitaji vifaa kama; muda, daftari, kalamu, n.k.

Utangulizi
Kuna aina mbalimbali za ripoti ambazo mwanafunzi wa kidato cha nne anatakiwa
kuziandika. Ripoti hizo ni muhimu sana kwa sababu zinamsaidia mwanafunzi katika
maisha yake ya baadaye. Katika somo hili, utajifunza namna ya kuandika ripoti.

Uandishi wa ripoti

Ripoti ni rekodi inayotolewa kama taarifa juu ya mtu, kitu au tukio fulani ambalo lime-
tokea, kwa mfano ajali, kifo,ziara, janga au maafa mengine.

Ripoti huandikwa kwa madhumuni ya kutoa taarifa ili taarifa hiyo iweze kufanyiwa kazi
au walau kuhifadhiwa kama kumbukumbu.

Muundo wa ripoti

Ripoti ni sharti iwe na sehemu kuu nne; sehemu hizo ni:

1. Kichwa cha ripoti/mada/anwani. Ripoti lazima iwe na kichwa cha habari; kichwa
hicho huandikwa kwa maneno machache. Mambo muhimu yanayotakiwa kuwepo katika
kichwa cha ripoti ni:

• Mahali pa tukio

• Aina ya tukio

• Tarehe ya tukio

• Muda wa tukio

2. Utangulizi wa ripoti. Utangulizi wa ripoti hueleza kwa muhtasari lengo la ripoti


kama ni kutoa taarifa au kumbukumbu. Majina ya wanajopo pia hutajwa kulingana na
idadi uliyopewa kwenye swali.

3. Kiini cha ripoti/mwili. Kiini cha ripoti kina maelezo yote kuhusiana na tukio lenyewe.
Sehemu hii huelezea kwa ufasaha mambo yaliyotokea, chanzo chake, ukubwa wake, wa-
husika, na tukio linalohusika.

4. Mwisho wa ripoti. Hii ni sehemu ya mwisho ya ripoti. Sehemu hii huonesha mambo
makuu mawili:

• Mapendekezo ya mwandishi wa ripoti.

• Jina la mwandishi wa ripoti (na cheo chake na mwenyekiti wa kamati.


Soma mfano huu wa ripoti

11
KISWAHILI | SENIOR FOUR

RIPOTI KUHUSU MGOMO WA WANAFUNZI KATIKA SHULE YA


SEKONDARI YA KACHUMBALI TAREHE 23/03/2020

Utangulizi

Kutokana na mgomo uliotokea katika Shule ya Sekondari ya Kachumbali, Ofisa wa Elimu


katika wilaya ya Kotido aliteua kamati tendaji ya watu watano ili wachunguze chanzo
cha mgomo huu. Kamati hii ilishirikisha watu wafuatao:
Mirembe Peace - Mwenyekiti
Matama Yohana - Katibu
Opio Badru - Mwanakamati
Nyakato Justine - Mwanakamati
Cheptegei - Mwanakamati

Kuhusu shule

Shule hii kirasmi ainaitwa Shule ya Sekondari ya Kotido. Ilianzishwa mwakani 1987
na sasa ina jumla ya wanafunzi elfu moja mia mbili. Inafundisha wasichana na wavu-
lana. Mwalimu mkuu wa Shule hii anaitwa Bi. Majaliwa Paskali na naibu wake ni Bw.
MashakaMengi. Idadi ya walimu ni sitini na watano na wafanyakazi wengine ni takribani
thelathini. Shule hii inapatikana wilayani Kotido.

Chanzo cha mgomo

Baada ya wanakamati kuwasiliana na wakazi jirani pamoja na wanafunzi kadhaa wa


shule hii, ilibainika kuwa sababu za mgomo shuleni zilikuwa:
1. Kuchelewa kwa matokeo ya mitihani.
Ilibainika kuwa wanafunzi walifanya mitihani katika mwezi wa Novemba na mpaka sasa
hawajapata matokeo yao. Mwalimu mkuu amewahi kuwatuma nyumbani wanafunzi ku-
leta karo ya shule lakini wakifika nyumbani wazazi wanaomba matokeo hayo. Hivyo wa-
nakamati waliona kuwa muda huu ni mrefu wakati ambapo matokeo yalihitajika.
2. Kuongeza karo maradufu
Wanakamati walipata taarifa kuwa katika kipindi cha miezi miwili katika muhula wa
tatu, karo ya shule ilikuwa imeongezwa mara mbili hata bila ya kuita wazazi kuambiwa
katika mkutano. Jambo hili lilileta vurugu miongoni mwa wanafunzi mpaka wakaamua
kuwalazimisha wakuu wa shule kuwaambia sababu zake.
3. Kula vibaya
Ilibainika kuwa tangu mwezi wa tisa, vyakula ambavyo vilistahili kuliwa na wanafunzi
havikupikwa tena jikoni. Hivi ni pamoja na mayai, chai ya maziwa, nyama na wali. Pia
ilibainika kuwa wanafunzi walipojaribu kuuliza sababu, Mwalimu mkuu hakusema lolote

12
SELF-STUDY LEARNING

jambo lililowakasirisha na wakakataa chakula.


Mapendekezo
Baada ya kamati kuchunguza sababu zilizochangia kuwepo kwa mgomo huu, ilipende-
kezwa kama ifuatavyo:
1. Kutoa matokeo ya mitihani
Mwalimu mkuu pamoja na walimu wafanye upesi iwezekanavyo watoe matokeo ya miti-
hani iliyofanyika katika mwezi wa Novemba.
2. Kuitisha mkutano wa wazazi
Mwalimu mkuu na wafanyakazi wengine wa shule wapange siku ambapo wataitisha
mkutano mkuu na wazazi wajadili karo inayofaa kulipiwa wala si kuongeza kila mara bila
ujuzi wa wazazi na wanafunzi.
3. Kurejesha upishi katika hali stahiki
Ni kitu muhimu kula vizuri. Pia, ni vyema wanafunzi walishwe kama wanavyolipa. Hivyo
wanafunzi wapewe vyakula wanavyovistahili, la sivyo waambiwe kwa nini chakula fulani
hakipo kwa wakati fulani ili wawe na uvumlilivu inapohitajika.
Tamati
Kamati hii ilifanya kazi yake kama ilivyohitajika na ingependa kushukuru Ofisa Elimu
katika wilaya ya Kotido kwa jukumu hili walilopewa. Shukrani ziwaendee wote walio-
fanikisha kazi hii.
Waandishi
. . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . .
Jina: Matama Yohana Jina: Mirembe Peace
Cheo: Mwenyekiti Cheo: Katibu
Tarehe: 17/8/2020Tarehe: 17/8/2020

Zoezi
1. Wanafunzi wa shule ya upili ya Kyamaneno wamefanya mgomo mbaya sana na
wamechoma nyumba ya mwalimu mkuu. Walimu mpaka sasa hawajajua chanzo
cha mgomo huo hatari. Afisa wa elimu katika wilaya ya Nakaseke ameteua kamati
ya watu watano na wewe ni katibu wao. Andika ripoti kuhusu chanzo cha mgomo
huo.
2. Katika kipindi cha miezi sita iliyopita, kumetokea ajali nyingi za barabarani katika
barabara ya kutoka Kampala kuelekea Masaka. Inspekta Mkuu wa polisi ameteua
kamati ya watu watano kufanya uchunguzi kuhusu chanzo cha ajali hizo na wewe
ndiye katibu wao. Andika ripoti kuhusu chanzo cha ajali hizo mbaya.
Funzo la tano: Kuandika insha ya kumbumbuku za mkutano

13
KISWAHILI | SENIOR FOUR

Umilisi:
Baada ya kujifunza somo hili, utaweza kuandika kumbukumbu za mkutano.
Utahitaji vifaa kama: muda, daftari, kalamu, n.k.

Utangulizi

Mwanafunzi wa kidato cha nne anatakiwa kuandika kumbukumbu za mkutano. Kumbu-


kumbu hizo ni muhimu sana kwa sababu zinamsaidia mwanafunzi katika maisha yake ya
baadaye. Katika somo hili, utajifunza namna ya kuandika insha ya kumbukumbu.

Kumbukumbu za mkutano

Kumbukumbu ni rekodi inayoonesha habari fupi za mazungumzo yaliyofanywa katika mkutano


ambazo ziliandikwa na kuhifadhiwa. Ni rekodi inayofanywa na katibu kuhifadhi mambo kamili
yaliyojadiliwa na kupishwa katika mkutano. Kumbukumbu huwa ni rekodi inayoonyesha
maendeleo ya kundi fulani kama kamati, bunge, walimu, nk inayoliwezesha kutimiza
mambo mbalimbali kama yanavyolengwa kutokana na vikao vyao. Kabla ya kuanzishwa
kwa mkutano au kikao chochote, kumbukumbu za mkutano awali hustahili kusomwa na
kuthibitishwa na wanakundi na mwenyekiti.

Kumbukumbu inakuwa na vipengele muhimu vifuatavyo:

i) Anwani/ kichwa. Kichwa kitoe jina la kikundi, mahali pa mkutano, tarehe na


saa za kikao/mkutano.
ii) Majina ya waliohudhuria na vyeo vyao vitajwe
iii) Waliokosa kuhudhuria kikao/mkutano kwa kutoa udhuru watajwe.
iv) Waliokosa kuhudhuria mkutano bila udhuru hufuata.
v) Walio katika mahudhurio pia huweza kutajwa yaani walikwa.
vi) Ajenda ya mambo ya kujadiliwa na kupishwa huorodheshwa.
vii) Wakati wa kuandika kumbukumbu, neno Kumb. (kifupi cha kumbukumbu)
huandikwa halafu nambari ya mkutano na mwaka. Kwa mfano Kumb. 01/2020
viii) Ajenda za mkutano huorodheshwa
ix) Utangulizi wa mkutano wakati mwingi huchukuliwa kama ajenda ambapo
mambo kuhusu maombi na kufungua kwa mwenyekiti hutajwa.
x) Kumbukumbu za mkutano wa awali husomwa na kuthibitishwa. Wanakamati
huunga mkono kumbukumbu hizi na kuwekewa Sahihi na mwenyekiti na katibu.
xi) Ajenda zilizotajwa hujadiliwa.
xii) Masuala yaliyoibuka kutokana na mada hutajwa na kujadiliwa.
xiii) Shughuli nyinginezo hufafanuliwa na kujadiliwa. Hizi huwa ni hoja zisizo na
uhusiano na ajenda za siku.
xiv) Kufungwa kwa mkutano ni kumbukumbu muhimu sana. Tarehe na saa ya mku-
tano utakaofuata hutolewa na baadaye maombi ya kufunga mkutano.
xv) Sehemu ya idhinisho huwekwa hatimaye. Jina la katibu, cheo, Sahihi na tarehe
hutolewa. Nafasi hii hutolewa kwa mwenyekiti.
xvi) Lazima Ikumbukwe kuwa hoja ndizo hujadiliwa wala siyo watu waliozitoa hoja
hizo.
Soma mfano huu wa kumbukumbu

14
SELF-STUDY LEARNING

KUMBUKUMBU ZA MKUTANO WA CHAMA CHA WANAFUNZI WA


KISWAHILI ULIOFANYWA KATIKA OFISI YA MWENYEKITI TARE-
HE 12/7/2020 SAA TANO ASUBUHI

Waliohudhuria
1. Okello Jude - Mwenyekiti
2. Atwine Dilan - Naibu Mwenyekiti
3. Yahaya Mohamed - Mweka Hazina
Waliotoa udhuru
1. Twesiime Richard - Naibu Katibu
2. Kabugho Rita - Mwanachama
3. Mahoro Irene - Mwanachama
Waliokosa kuhudhuria bila udhuru
1. Chesang Betty - Mwanachama
2. Osele Nicho - Mwanachama

Ajenda
1. Kufunguliwa kwa mkutano
2. Kusomwa na kuthibitishwa kwa kumbukumbu za mkutano wa awali
3. Yaliyotokana na kumbukumbu hizo.
4. Miradi ya Chama.
5. Maandalizi ya Kongamano
6. Shughuli nyinginezo.

Kumb: 01/2020 Kufunguliwa kwa mkutano

Mkutano ulifunguliwa kwa maombi saa tano kamili asubuhi. Mwenyekiti aliwashukuru
wanachama kwa kuhudhuria kwao na kuwafahamisha kuwa kulikuwa na mhadhiri mgeni
mlezi wa Chama cha Wanafunzi wa Kiswahili, Bi. Asiimwe Phionah. Kisha aliwaomba
wanachama wamuunge mkono ili chama kiendelee.
Kumb: 02/2020 Kusomwa na kuthibitishwa kwa kumbukumbu za mkutano wa awali
Kumbukumbu za mkutano uliotangulia zilizosomwa na katibu Ojok Peter na kuthibitish-
wa na wanachama kuwa zilikuwa rekodi kamili ya mambo yaliyozungumziwa na hivyo
kuidhinishwa na mwenyekiti na katibu wake.
Kumb: 03/2020 Yaliyotokana na kumbukumbu hizo
Kwa kuwa hakukuwa na mengi yaliyotokana na mkutano uliotangulia, katibu aliomba
wanachama waendelee na ajenda za siku.

Kumb: 04/2020 Miradi ya Chama.


Wanachama walikubaliana kuchangia kiasi cha pesa shilingi elfu kumi kwa ajili ya ku-

15
KISWAHILI | SENIOR FOUR

endesha miradi yao. Pia, walikubaliana kuwa wasajili wanachama wengine kumi ili wapa-
te pesa zaidi za kuendesha shughuli za chama. Aidha, walikubaliana kuwa waanzishe
mradi mpya wa kuuza vitabu vya Kiswahili ili wapate kipato zaidi.
Kumb: 05/2020 Maandalizi ya Kongamano
Wanachama walikubaliana kuwa kongamano la Kiswahili la kitaifa lizungumziwe katika
mkutano utakaofuata. Mlezi wa Chama aliungwa mkono wazo hili na hivyo kongamano
litazungumziwa leo.
Kumb: 06/2017 Shughuli nyinginezo
Ilipitishwa kuwa:
(a) kila mwanakamati ashawishi watu watano waingie katika chama
(b) kila mwanachama atafute michango kutoka nje ya chuo ili wapate usaidizi wa kiu-
chumi.
Kumb: 07/2020 Kufungwa kwa mkutano
Kwa kuwa hapakuwa na jingine la ziada, mkutano ulifungwa kwa maombi kutoka kwa
Kayihura Ismael saa saba za mchana.
Thibitisho
Mwenyekiti ………………………. Sahihi …………………… Tarehe
………………… Katibu ………………………… Sahihi …………………….
Tarehe …………………
Zoezi
Wewe ni katibu mkuu wa Chama cha Wazalendo shuleni mwako, ziandike kumbukumbu
za mkutano uliokuwepo tarehe 2 Machi mwaka huu ambao uliuhudhuria. Tumia maneno
yasiyopungua 150 wala kuzidi maneno 250.

Shughuli 3.4: Maswali kuhusu uandishiwa insha mbalimbali


Tunga insha mbili fupifupi miongoni mwa mada zifuatazo. Kila insha isipungue maneno
150 wala kuzidi 200.
i. Tangazo la kifo
Familia ya Mzee Alfred Ihoora, wanasikitika kutangaza kifo cha Mzee wao marehemu
Alfred Ihoora, aliyefariki jana jioni tarehe sita mwezi wa Julai 2020. Mazishi yatafanyika
kesho saa saba mchana nyumbani kwao kijijini Kigoma wilayani Bushenyi. Ndugu, jamaa
na marafiki mnatangaziwa popote pale mlipo.
a. Andaa ratiba ya mazishi ya Mzee Alfred Ihoora.
b. Wewe ni Mwalimu mkuu wa shule ya Chekechea ya Kigoma. Andika ujumbe wa
rambirambi kwa familia ya Mzee Alfred Ihoora.
ii. Mahabusu alitoroka gerezani na kabla ya kufika mbali, akakutana na Askari mkuu
wa Jela. Akakamatwa na kurejeshwa kwa Askari aliyekuwa kwa zamu. Andika ma-
zungumzo miongoni mwa watu hawa watatu baada ya kufika ofisini mwa Askari
aliyekuwa kwa zamu.

16
SELF-STUDY LEARNING

iii. Andika hotuba ya:


a. Afisa wa afya kwa wanakijiji kuhusu Virusi vya Korona.
b. Mwalimu mkuu katika sherehe ya kukaribisha wanafunzi wa kidato cha
kwanza na cha nne.
c. Chifu kwa wanakijiji wake kuhusu uraibu wa mihadarati.
iv. Rafiki yako wa muda mrefu ambaye anaishi Marekani anapanga kurudi Uganda.
Anapendekeza kukuzuru shuleni katika siku ya wageni lakini hajui mahali shule
yako ilipo. Andika barua pepe kumwelekeza jinsi ya kufika shuleni kwako kutoka
kituo cha ndege cha Entebbe. Chora ramani kuonesha mahali shule yako ilipo ku-
toka kwa kituo cha biashara kilicho karibu.
v. Msanii Diamond Platinumz anapanga kuja Uganda na aimbie katika ukumbi wa
Freedom City. Andika tangazo ukiwaarifu wapenzi wa muziki wa kizazi kipya
kuhusu mpango huo.

Muhtasari wa mada
Je, unakumbuka kuwa katika mada hii umejifunza kuhusu, kuandika aina mbalimbali za
insha? Ujuzi huu utakusaidia kuimarisha mawasiliano yako katika lugha ya Kiswahili.

Mada Kuu 3: Ufupisho

Funzo/somo: Kufupisha makala mbalimbali

Umilisi:
Baada ya kujifunza somo hili utaweza:
i) Kutambua utaratibu wa kufupisha makala.
ii) Kufupisha makala mbalimbali kwa kufuata utaratibu mwafaka.
Utahitaji vifaa kama; muda, daftari, kalamu, n.k

Utangulizi

Je, ulikuwa unajua kuwa neno ufupisho linatokana na neno ‘fupisha’ lililo na maana
ya kupunguza urefu? Katika muktadha wa shuleni, neno ufupisho linamaanisha kutoa
muhtasari wa maudhui husika au taarifa uliyopewa. Katika funzo hili, utajifunza kuhusu
kufupisha makala mbalimbali.

Maagizo: Tafuta pahali mwafaka kusoma makala haya. Utafanya mazoezi na shughuli zote
zilizomo. Kumbuka kuwa baadhi ya shughuli zinaweza kuchukua muda mrefu. Soma maagizo
kwa makini kabla ya kufanya zoezi/shughuli husika.
Ufupisho
Ufupisho ni hali ya kutoa muhtasari wa maudhui ya makala au habari fulani. Kwa mfano
habari yenye aya ishirini au zaidi yaweza kupunguzwa urefu hadi aya moja yenye ma-
neno yasiyozidi mia. Ufupisho siyo tu kupunguza urefu au idadi ya maneno katika ibara
iliyopewa. La hasha! Wakati wa kufupisha, unastahili kutafuta hoja muhimu au maudhui

17
KISWAHILI | SENIOR FOUR

muhimu na kutupa hoja zisizo na uzito.


Shughuli 4.1: Kutambua utaratibu wa kufupisha makala
1. Kariri utaratibu ufuatao unaofaa kuzingatia wakati wa kufupisha taarifa ya
habari.
Wakati unapoanza mchakato wa ufupisho, unastahili kuzifikiria hoja zifuatazo kama
mwongozo wa ufupisho:
1. Kwanza kabisa, soma swali zaidi ya mara moja upate nini unachoelekea kufupi-
sha.
2. Soma habari/makala uliyopewa mara mbili au tatu na uzipigie mistari hoja
muhimu.
3. Orodhesha hoja (vidokezo) ulizopata katika ibara nzima.
4. Viandike vidokezo (hoja) ulizooodhesha hapo juu katika muhtasari wenye mtiririko
na mshikamano kulingana na ibara.
5. Andika nakala chafu katika aya moja. Tumia maelezo yako mwenyewe.
6. Hesabu maneno uliyo nayo ili upate kulinganisha na yale yanayohitajika.
7. Soma tena nakala yako chafu huku ukiondoa maneno yasiyo na maana, kuandika
visawe vya maneno marefu au kuongeza maelezo yako mwenyewe kulingana na
idadi ya maneno unayohitaji.
8. Andika nakala safi. Tumia mwandiko unaoweza kusomeka.
9. Hesabu maneno tena na uandike idadi chini ya nakala yako ya mwisho. Si lazima
idadi iwe ileile ya mtahini lakini afadhali uwe upungufu wa maneno kati ya matano
na kumi.

Mfano;

Fuata utaratibu mwafaka kufupisha aya hii katika maneno yasiyozidi 20.
Ajali ni tukio linalotokea kwa ghafla. Ajali ni kitu kinachotokea bila kupangwa wala
kutarajiwa. Tukio hili aghalabu husababisha madhara au hatari. Waathiriwa wa ajali
hupatwa na matata kama maumivu, kupoteza viungo fulani vya mwili kama mikono, mi-
guu miongoni mwa vingine. Ajali inaweza kutokea wakati mtu anasafiri, akiwa amelala,
akiwa ameketi na katika hali yoyote ile anayekuwemo.
Vidokezo
-Ajali ni tukio la ghafula.
-Hutokea bila kupangwa
-Husababisha madhara/hatari kv; maumivu, kupoteza viungo vya mwili, n.k.
-Ajali hutokea wakati wowote.
Nakala chafu
Ajali ni tukio la kighafula linalotokea bila kupangwa. Ajali husababisha madhara kama
maumivu, kupoteza viungo vya mwili. Ajali inaweza kutokea wakati wa kusafiri, kulala,
kuketi na katika hali yoyote ile.
Nakala safi

18
SELF-STUDY LEARNING

Ajali ni tukio la kighafula. Husababisha madhara kamakupoteza viungo vya mwili. Ajali
inaweza kutokea wakati wowote ule.
(Maneno 18)
Zoezi: Kufupisha makala
1. Fupisha makala yafuatayo kwa maneno 100.

Siku moja punda wa Abunuwas alikuwa na kiu. Kitu cha kumtilia maji apate kunywa hana.
Akaenda kwa jirani yake, akamwambia, niazime sufuria yako nimnyweshee punda wangu
maji. Yule jirani akampa Abunuwas sufuria, akaenda zake. Akakaa nayo siku ya kwanza,
siku ya pili, siku ya tatu. Siku ya nne, akaamua kutwaa ile sufuria kwa mwenyewe, akatia
na kisufuria kidogo ndani, akampelekea mwenyewe.
Abunuwas alipofika kwa jirani yake, akamwambia, sifuria yako ndiyo hii hapa.
Akaitwaa, akaona ndani kisufuria kidogo, akanena, Hiki kisufuria kidogo si chetu.
Abunuwas akanena, mimi si mwizi siwezi kuiba mali ya watu; sufuria yako imezaa kwan-
gu, na huyu mtoto wake. Yule mwenye sufuria akafurahi sana, akanena, Nyumba ya
Abunuwas ina baraka sana, inazaa hata sufuria.
Hata siku ya tatu akaenda kuiazima sufuria ile ile. Akapewa. Na safari hii Abunuwas
akakaa nayo hakuirudisha. Mwenye sufuria akaenda kuuliza kwa Abunuwas sufuria
yake. Abunuwas akanena, sufuria yako imekufa. Yule akanena, Shaba hufa? Abunuwas
akanena, Haikuzaa? Akanena, ilizaa. Abunuwas akanena, Kila kitu kinachozaa, hatima
yake hufa. Akashindwa kumjibu. Akawauliza wanachuoni habari hii, wakamjibu vile vile,
hakika kinachozaa na kufa hakina budi. Abunuwas akahodhi sufuria.

Muhtasari wa mada
Je, unakumbuka kuwa katika mada hii umejifunza kuhusu, kufupisha makala mbalimbali
kwa kuzingatia hoja muhimu. Ujuzi huu utakufaa katika maisha yako ya kila siku.

19
KISWAHILI | SENIOR FOUR

Mada Kuu 4: Tafsiri

Funzo/somo: Kutafsiri makala mbalimbali

Umilisi:
Baada ya kujifunza somo hili utaweza:
i) Kutambua utaratibu wa kutafsiri makala.
ii) Kutafsiri makala mbalimbali kwa kufuata utaratibu mwafaka.

Utahitaji vifaa kama: muda, daftari, kalamu, n.k

Utangulizi

Unajua kuwa tafsiri ni muhimu katika maisha yetu? Tafsiri ni muhimu kwani husaidia ku-
fanikisha mawasiliano, kufanikisha ushirikiano kibiashara, kisiasa, kielemu, kitamaduni
n.k. Aidha tafsiri ni njia ya ajira. Katika somo hili, utajifunza namna ya kutafsiri makala
mbalimbali katika lugha ya Kiswahili.

Maagizo: Tafuta pahali mwafaka kusoma makala haya. Utafanya mazoezi na shughuli zote
zilizomo. Kumbuka kuwa baadhi ya shughuli zinaweza kuchukua muda mrefu. Soma maagizo
kwa makini kabla ya kufanya zoezi/shughuli husika.
Tafsiri
Tafsiri ni shughuli ya kuhamisha mawazo katika maandishi kutoka lugha moja hadi
nyingine. Kutafsiri ni kuchukua mawazo yaliyo kwenye maandishi kutoka lugha chanzi
na kuyawasilisha katika lugha lengwa.
Aina za tafsiri
Kuna aina mbalimbali za kufanya tafsiri. Kila aina ina sifa zake, ufaafu wake na upun-
gufu wake.

Shughuli 5.1 Kutambua aina za tafsiri


1. Kariri aina zifuatazo za tafsiri.

i) Tafsiri sisisi. Hii ni mbinu ya kutafsiri neno kwa neno. K.m;


-The teacher told the students to pull up their socks.
-Mwalimu aliwambia wanafunzi kuvuta soksi zao juu.
ii) Tafsiri maana. Mbinu hii ya tafsiri huzingatia maana ya sentensi husika. Pia hii
hurejelewa kama tafsiri ya kisemantiki.k.m;
-The teacher told the students to pull up their socks.

20
SELF-STUDY LEARNING

-Mwalimu aliwashauri wanafunzi kutia bidii katika masomo yao.


Shughuli 5.2: Kutambua utaratibu wa kutafsiri

1. Soma kwa sauti na kisha utafakari juu ya utaratibu ufuatao wa kutafsiri:


1. Soma kwa makini makala ya kutafsiri zaidi ya mara moja.
2. Mawazo katika lugha chanzi na lengwa sharti yalingane.
3. Ni muhimu mtafsiri azingatie muktadha, muundo, mtindo wa lugha na
utamaduni. Athari za vipengele hivi zinaweza kusababisha upungufu katika
tafsiri. K.m,
4. Matumizi ya lugha sanifu na iliyo sahihi kisarufi.
Shughuli 5.3: Kutafsiri makala

Tafsiri habari hii katika Kiswahili sanifu.


My school life
My name is Nakafeero Mariam a daughter of Mr. KafeeroMohamed. My mother is Mrs.
Anyango Sarah. We stay in Kiswera village, Nakawa Division Kampala district. I am six-
teen years old and I study from Nyati High school.
I am in Form Four and my best subject is Kiswahili language. In our class we are fifty
four students and all are girls. Our school is a single school for only girls. It has about
one thousand three hundred students in total. Our school has six classes that is senior
one to senior six.
Our school has sixty teachers and all of them are very good teachers. Our head teacher
is a very smart lady who cares about us so much. I am a very serious student at school
and all teachers like me because i perform well academically.

Muhtasari wa mada

Je, unakumbuka kuwa katika mada hii umejifunza kuhusu, kutafsiri makala mbalimbali
kutoka kwa lugha ya Kiingereza hadi lugha ya Kiswahili.

21
KISWAHILI | SENIOR FOUR

Mada Kuu 5: Malipo

Funzo/somo: Msamiati wa malipo mbalimbali.


Umilisi: Baada ya kujifunza somo hili utaweza;
i). Kutambua msamiati wa malipo mbalimbali.
ii). Kutumia msamiati wa malipo katika sentensi.
Utahitaji vifaa kama; muda, daftari, kalamu, n.k

Utanguliz
i
Unajua kuwa ni muhimu kujua msamiati wa malipo mbalimbali katika maisha yetu?
Msamiati wa malipo ni muhimusana kwa sababu husaidia kuimarisha mawasiliano yetu
pindi tunapokuwa tunafanya shughuli mbalimbali za kijamii, kiuchumi, n.k.

Maagizo: Tafuta pahali mwafaka kusoma makala haya. Utafanya mazoezi na shughuli
zote zilizomo. Kumbuka kuwa baadhi ya shughuli zinaweza kuchukua muda mrefu. Soma
maagizo kwa makini kabla ya kufanya zoezi/shughuli husika.

Malipo

Malipo ni kitu ambacho hutolewa na mtu ili kugharamia shughuli fulani. Malipo pia huit-
wa ada.

Shughuli 6.1: Kutambua msamiati wa malipo

1. Soma msamiati wa malipo ufuatao:

Msamia- Maana Matumizi katika sentensi


ti
Karo Ada ya shule inayotolewa na Baba amenilipia karo
mwanafunzi
Nauli Malipo ya kusafiria Sina nauli ya kwenda nyumbani
Mahari Malipo ya kuolea Bwana arusi ametoa mahari
Fidia Malipo kwa kusababishiwa hasara Mzee Yakobo alipewa fidia baada ya kush-
au maumivu inda kesi
Riba Malipo kwa mkopo Mkopo huu una riba kubwa

22
SELF-STUDY LEARNING

Arbuni Malipo ya kwanza ya kununulia Nimetoa arbuni kwa ng’ombe huyo


kitu au kufungia kitu kisinunuliwe
na mwingine
Mshahara Malipo ya mfanyakazi ya kila Walimu wanapata mshahara mzuri
mwezi
Faini Pesa za adhabu kwa kosa Tuliambiwa kulipa faini baada ya kuchelewa
kufika
Kiingilio Ada ya kuingilia michezoni/mata- Mama amenilipia kiingilio kwa ajili ya mbio
mashani za magar
Pensheni Malipo ya kustaafu Babu yangu anapata pensheni
Mchango Ada ya hiari ili kufanya shughuli Wazazi waliomba mchango wa chakula
fulani
K i o k o z i / Ada ya kukombolea kitu kili- Tunataka kombozi ili kumwachilia mtoto
kombozi chotekwa nyara wako
A j a r i / Malipo kwa muda wa ziada wa ku- Walimu wanadai ovataimu yao
ovataimu fanya kazi
Dhamana Ada itolewayo na mshtakiwa Matayo ameachiliwa kwa dhamana ya laki
kabla kesi yake ikatwe moja
Koto Ada ya kumwingiza/kumsajili Je, mwaka huu tutalipa koto ya shilingi nga-
mwanafunzi shuleni pi?
Pango Kodi ya nyumba/chumba anayoli- Wapangaji wameshindwa kulipa pango kwa
pa mpangaji kila mwezi sababu ya Virusi vya Korona

Shughuli 6.2: Kueleza maana ya msamiati wa malipo

1. Eleza maana ya malipo yanayooneshwa katika jedwali lifuatalo.

Msamiati wa malipo Maana


Kodi ya mapato Malipo kwa serikali kulingana na mapato ya mtu
Marupurupu
Urithi
Kiangazamacho
Masurufu
Riba

23
KISWAHILI | SENIOR FOUR

2. Tunga sentensi sahihi kwa kutumia msamiati ufuatao wa malip


Karo . . . . . . . . . . . . . . . ... . .. . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . .
Fidia . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . .
Nauli . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . .
Ushuru wa forodha . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . .
Mahari . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . .

3. Toa jibu sahihi kwa maswali yafuatayo:


a. Kodi ya nyumba inaitwaje? . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . .. . . . .
b. Malipo ya kujiunga na Chuo kikuu ni? . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . .
c. Pesa mtu atumiazo kuanzisha biashara huitwaje? . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . .
d. Malipo ya kuingiza bidhaa nchini huitwaje? . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . .
e. Malipo ya kusafiria ni? . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . .. . . . . . . . . . .

Muhtasari wa mada

Je, unakumbuka kuwa katika mada hii umejifunza kuhusu malipo mbalimbali? Msamia-
ti huu wa malipo utakusaidia kuimarisha mawasiliano yako katika lugha ya Kiswahili.

Sherehe
Biashara: Ununuzi na uuzaji wa bidhaa.
Chekechea: shule ya watoto wadogo aghalabu wenye umri usiozidi miaka mitano.
COVID-19: Ugonjwa unaosababishwa na virusi vya Korona. Ulianzia Uchina mwezi
wa Desemba 2019 na kuenea duniani kote. COVID ni kifupi cha Corona
virus Disease na 19 hurejelea mwaka ugonjwa huu ulipozuka yaani 2019.
Kipato: Mavuno au fedha anazopata mtu kutokana na kazi anayoifanya au faida
ya mauzo ya kitu.
Korona: Virusi vinavyosababisha ugonjwa wa COVID-19.

Lugha: Mpangilio wa sauti na maneno unaoleta maana ambao hutumiwa na

binadamu kuwasiliana.

Mawasiliano: Upashanaji habari kwa njia mbalimbali.


Ratiba: Mpango wa mfululizo wa mambo yanayofanyika au yatakayofanyika

24
SELF-STUDY LEARNING

wakati fulani. Panga ratiba ya masomo.

Rithi: Pata/miliki kitu kutoka kwa aliyekufa. Akello alirithi mali nyingi.

Tamasha: Sherehe au mambo yanayofanywa kusherehekea tukio fulani zuri.


Vifaa/kifaa: Kitu au chombo kinachotumika katika kufanyia kazi au kutekeleza

25
National Curriculum
Development Centre,
P.O. Box 7002,
Kampala.

www.ncdc.go.ug

You might also like